Sunday, May 27, 2012

Picha Mbalimbali za Maandamano Visiwani Zanzibar Yaliyozua Taharuki na Hali Tete

 Mmoja
wa waandamani wa Kundi la Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam
(JUMIKI) Kisiwani Unguja,Zanzibar akionyeshan kitambaa kilicho na Damu
mapema leo Asubuhi wakati wakiendelea na maandamano yao ambayo
yamesababisha vurugu kubwa kisiwani humo,iliyopelekea kuchomwa moto kwa
moja ya makanisa pamoja baadhi ya magari yaliyokuwa yameengeshwa karibu
na njia wapitazo.vurugu hizo zimeanza jana usiku baada ya kukamatwa kwa
kiongozi wa Juimuiya hiyo
 Maelfu
wa wazanzibari wakiongozwa na Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho
na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) wakifanya matembezi ya
amani katika barabara za Zanzibar na kupeleka ujumbe wao kwa viongozi
wa serikali za Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
pamoja na Umoja wa Mataifa wakitaka Zanzibar huru ambapo baadhi ya
watembeaji hao wakiongoza na Kiongozi wa Jumuiya hizo, Sheikh Farid
Hadi Ahmed na viongozi wengine
 Kikosi
cha Kuzuwia Fujo FFU kikizunguka kikiwa kimejihami katika maeneo ya
Michenzani ambapo tayari jeshi la polisi limepiga marufuku mikusanyiko
yoyote Mjini hapa
Katibu
wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) Sheikh
Abdallah Said Ali ambaye ni miongoni mwa wanaotafutwa na jeshi la
polisi akizungumza na Radio DW asubuhi mapema kabla ya taarifa ya
kutafutwa kwao kutolewa kwa vyombo vya habari
---
Maelfu
ya wazanzibari leo wamefanya maandamano amani kuishindikiza Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar kuitisha kura ya maoni juu ya Muungano na
kupeleka ujumbe kwa Umoja wa Mataifa wa kutaka Zanzibar kujitenga kama
ilivyofanya Sudan ya Kusini.


Wazanzibari
hao wakiongozwa na Sheikh Farid Hadi Ahmed walitembea kutoka viwanja
vya Lumumba na kupitia barabara ya Kinazini, Mpigaduri, Michenzani
Maskani ya CCM Kisonge, kwa Biziredi na kurudi tena viwanja vya
Lumumba.


Maandamano
hayo walioyaita matembezi ya amani yalifanyika na kuhudhuriwa na
maelfu ya wazanzibari ambapo awali kuliandaliwa kongamano kubwa
lililoandaliwa na Taasisi za Kiislamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya
Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa lengo la
kuzungumzia mfumo wa elimu Zanzibar.


Akizungumza
na maelfu ya wazanzibari kabla ya kuanza maandamano hayo yaliitwa ni
matembezi ya amani, Sheikh Farid alisema wazanzibari wana haki kama
walivyokuwa na haki wananchi wengine ulimwenguni kote kudai haki yao
ndani ya nchi yao.


“Sisi
wazanzibari kama wananchi wengine wowote duniani tuna haki ya kikatiba
kudai nchi yetu kama walivyodai Sudan ya Kusini, mbona Sudan ya
wameweza kujitenda na kupata nchi yao kwa nini sisi kama wazanzibari
tusikubaliwe kudai nchi yetu sasa sisi tunampelekea salam katibu mkuu
wa umoja wa mataifa kumwambia kuwa wazanzibari sasa wanataka nchi yao”
alisisitiza Sheikh Farid huku akiungwa mkono kwa mamia hao kuinua
mikono na kusema ndiooooo.


Awali
Sheikh Farid alisema salamu hizo anataka zimfikie Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa Ban Kin moon ambaye kwamba wazanzibari wamechoshwa na
kuwepo ndani ya Muungano ambao umedumu kwa miaka 48 lakini bado ukiwa
na kero nyingi na malalamiko ambayo yanaonekana utatuzi wake ni mdogo
na usiowezekana ambapo alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hauna
manufaa yena na wazanzibari.


Katika
kuonesha kwamba hawataki tume ya katiba ije kuchukua ya maoni ya
katiba mpya Sheikh Farid alisema wanataka kwanza kuamuliwe suala la
Muungano kabla ya jambo lolote na kuahidi kwamba wataendelea kufanya
makongamano, mihadhara na maandamano kwa kadiri wawezavyo hadi hapo
serikali itakaposikia kilio hicho.


“Ujumbe
huu tunautoa kwa Ban Kin moon, na kwa ulimwengu mzima lakini pia
tunataka rais wetu Dk Shein asikie kilio hiki na Rais Kikwete ambaye
yeye ni mtetezi wa haki za binaadamu na pia ni mfuatiliaji wa nchi
zinazovunja haki za binaadamu tunataka asikie kilio cha wazanzibari
kuwa wanataka nchi yao” alisema. 


Alisema
juzi wamefanya maombi maalumu ya kumuombea Rais wa Zanzibar lengo
likiwa ni kumjaaliwa kheri na awe na maamuzi sahihi juu ya wananchi wa
Zanzibar sambamba na kuwaomba Makamu wa Kwanza na makamu wa Pili wa
Zanzibar kusikia kilio cha wazanzibari wasiotaka Muungano.


“Tunamuomba
Rais wetu Dk Shein, Makamu wa Kwanza Maalim Seif na Makamu wa Pili
Balozi Seif kwamba sisi wazanzibari tunahitaji Zanzibar huru,
tunahitaji heshima ya nchi yetu na tupo tayari kwa lolote kwa hivyo
tunataka salamu hizi na ujumbe huu ukufikieni” alisema Sheikh Farid
huku akiungwa mkono na maelfu waliohudhuria katika kongamano hilo
ambalo awali liliandaliwa kwa lengo la kuzungumzia masuala la elimu na
mfumo wake.


Akiendelea
kutoa salamu hizo mara Sheikh Farid alisoma kifungu cha 16 cha katiba
na kuwaleza wananchi kwamba haki ya kutembea ni haki ya kila mwananchi
ambayo imeainishwa katika katiba na sheria za haki za binaadamu hivyo
aliwageukiwa na kuwataka wasimame na kisha kumfuata yeye.


“Haki
ya kutembea ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria na kifungu cha 16
kinatupa haki ya kutembea sasa mimi nataka kutembea jeee mpo tayari
kutembea na mimi? Alihoji Sheikh huyo huku akijibiwa na umma mkubwa
kwamba ndioooo”


Aliongeza
kwamba “Tunaanza kutembea na tuone mtu atukamate tunakwenda njia ya
kinazini, tunapita michenzani, tunapita barabara ya kwa biziredi na
kisha tunarejea hapa hapa kuendelea na kongamano letu kwa amani kabisa
mmesikia….akajibiwa ndiooooo”
baada
ya kusema hivyo Sheikh Farid alitoa takbir na kuanza kukamatana mikono
na viongozi wenzake na huku ummati mkubwa ukiwa umekamatana mikono
nyuma na kuanza safari kwa pamoja na kutembea katika barabara ambazo
walizitaja awali.


Waandamani
hao walikamata mabango yenye maandishi mbali mbali ikiwemo hatutaki
muungano, tunataka nchi yetu, zanzibar bila ya muungano inawezekana na
wengine kadhalika huku wakitembea njiani na kupiga takbir ambapo
walikuwa wakisema Mwenyeenzi Mungu Mkubwa, Mwenyeenzi Mungu Mkubwa sisi
hatuna uwezo isipokuwa tunakutegemea wewe Mwenyeenzi Mungu.


Waandamanaji
hao walianza kutembea kwa utaratibu maalumu huku magari yakisimama na
kuwapisha bila ya kuwepo jeshi la polisi ambapo viongozi wa jumuiya
hiyo na wananchi wengine waliongoza utaratibu huo na kutembea katika
barabara kwa utaratibu mzuri hadi kumaliza maandamano yao waliyoyaita
matembezi ya amani. 


Baadae
jeshi la polisi lilifika katika eneo ambalo kumefanyika maandamano
hayo na kufungua mabango yao ya kuwataka watu kuondoka lakini wakati
magari hayo ya polisi matatu yanafika eneo hilo la Kariakoo tayari
ummati mkubwa ulikuwa umeshapita katika eneo hilo na hivyo kuingia
ndani ya magari yao na kuondoka kwa salama.


Awali
akitoa mada katika kongamano hilo, Maalim Abdulhafidh Malelemba
alisema sekta ya elimu imekuw aikidorora Zanzibar kutokana na
kukandamizwa na mambo ya Muungano ambapo kila mwaka wanafunzi
wanapofanya mitihani kufelishwa kwa makusudi huku idadi ya wanafunzi
wanaokwenda katika vyuo vikuu wakiwa kidogo kutokana na kufelishwa
katika mitihani ambapo husainiwa na baraza la mithani Tanzania (NECTA).


Wakizungumza
katika nyakati tofauti katika kongamano hilo, baadhi ya walimu
walisema kukosekana kwa baraza la mitihani Zanzibar kusimamia mitihani
ya elimu ya juu ndio sababu ya wazanzibari kufelishwa kwa wingi na
kushindwa kuingia katika vyuo vikuu kwa kuwa wanafunzi wengi wa
Zanzibar hufelishwa.


Walimu
hao walitoa ushahidi wa hivi karibuni wa kufelishwa wanafunzi wa
kidatu cha nne ambapo walisema lile ni tukio la makusudia lililofanywa
na baraza la mitihani ikiwa ni kuwadhoofishwa wanafunzi wa Zanzibar ili
wasiendelee katika masomo kwa kuwafelisha.

Kwa hisani ya Zanzibar yetu.

Saturday, May 26, 2012

CHADEMA yafunika Dar




MBOWE AKEMEA WANAOENEZA UDINI, UKABILA
LICHA ya Jeshi la Polisi kutoa amri wananchi na wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam wasiandamane kuelekea katika viwanja vya Jangwani jana kuhudhuria mkutano wa hadha ra wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), viwanja hivyo vilifurika umati wa wananchi kwa kiasi kikubwa huku utulivu ukitawala.
Umati huo ulianza kuingia uwanjani hapo majra ya asubuhi huku kukiwa na vibanda 16 vilivyokuwa vikisimamiwa na vijana kutoka vyuo vikuu ambao ni wanachama wa CHADEMA kwa ajili ya watu kujiunga na chama hicho na wengine kurudisha kadi za vyama vingine.
Kutokana na zoezi hilo la kurudisha kadi na kupata wanachama wapya, jumla ya watu 3,124 walijiunga na CHADEMA jana katika viwanja hivyo akiwamo mzee Raphael Koimere, aliyekuwa kada maarufu wa CCM.
Majira ya saa 9:20 mchana msafara wa wapanda pikipiki zaidi ya 200 uliwasili uwanjani hapo huku wengine wakiwa na mabango ya kuhamasisha na kuelezea kasoro za kufanyiwa kazi.
Miongoni mwa mabango hayo yaliyosema: ‘Jimbo la Ilala linawaangusha Watanzania katika mageuzi ya kweli kwa kuwa mipango yote ya ufisadi huanzia hapo na kutekelezwa katika ofisi zilizo katika wilaya hiyo’.
Mabango mengine yalisomeka: ‘Shibuda ulikuja CHADEMA kwa mkopo na sasa hatukutaki, rudi ulikotoka’, ‘Tunamuomba CAG akague hesabu katika ofisi za mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala na jingine likiwatahadharisha CCM muda wao wa kuwa madarakani umekwisha waanze mazoezi ya kuwa wapinzani wa kudumu, kama si kupotea katika ramani ya kisiasa ya Tanzania.
Majira ya saa 9:30 mchana viongozi mbalimbali wa CHADEMA walianza kuwasili uwanjani hapo wakiwamo wabunge wa chama hicho wakiongozwa na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo.
Baadhi ya viongozi waliowasili uwanjani hapo ni pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema, wanasheria maarufu nchini Mabere Marando, Profesa Abdallah Safari na Edson Mbogoro, huku wanachama waliojiunga na CHADEMA hivi karibuni kutoka mkoani Arusha James ole Milya na Ally Bananga wakiwa ni miongoni mwa watu waliokaa meza kuu.
Ilipofika saa 9:54 Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA aliwasili uwanjani hapo huku akifuatiwa na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa, hali iliyoamsha shangwe kubwa kutoka kwa wananchi waliokusanyika uwanjani hapo.
Baada ya kuketi viongozi hao, mkutano ulifunguliwa kwa dua kutoka kwa viongozi wa dini ya Kiislamu na Kikristo na kisha baadhi ya viongozi wakaanza kuzungmza huku viongozi watatu wakiwa ndio wasemaji wakuu katika mkutano huo, ambao ni Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu.
Mbowe akemea udini, ukabila
Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, akihimiza kuwekwa mbele kwa masilahi ya taifa badala ya vikundi vya watu wachache.
Alisema ni wakati wa Watanzania kutambua haki zao na kuwaonya viongozi wa serikali ili kuacha mtindo wa kuligawa taifa kwa dhana ya udini, ukabila na ukanda.
“Ninaliongea hili kwa kuwa kuna watu sasa hawajui hatima yao na wamebaki katika kukumbatia suala zima la udini, ukanda na ukabila kuligawa taifa, mimi ninawaambia Watanzania, sisi CHADEMA kama chama kinachojipanga kuchukua dola tunamhitaji kila mmoja mwenye sifa ya Utanzania, pasipo kujua dini yake, kabila lake, wala anatoka ni eneo gani la nchi,” alisema Mbowe.
Akizungumzia utata wa kauli mbalimbali za baadhi ya wanachama ndani ya CHADEMA, Mbowe alisema hawataweza kumvumilia mtu yeyote mwenye dhamira ya kuvuruga umoja ndani ya chama hicho kwa masilahi yake na kundi lake.
Akizungumza kwa hisia kali, pasipo kutaja jina la mtu, licha ya maongezi hayo kuonekana yakimlenga Mbunge John Shibuda, Mbowe alisema: “Hatua ya kuifikisha CHADEMA hapo ilipo ilianza miaka 20 iliyopita na kwamba akitokea mtu wa kuivuruga, taratibu za kumuwajibisha zitafuatwa.
“Kauli ya chama ni makini, hakitayumbishwa na propaganda za mapandikizi na hata wasio na nia nzuri na nchi. Tutafanya maamuzi mazuri kwa njia ya haki na tusimfikirie mpuuzi mmoja kutuharibu, yeyote atakayechezea moto utamchoma,” alisema Mbowe.
Akilizungumzia Jeshi la Polisi na hali ya amani, Mbowe alisema jeshi hilo liache kutumika kwa masilahi ya CCM na badala yake lifanye kazi kwa maadili ya jeshi hilo.
Alisema licha ya uchokozi unaofanywa mara kwa mara na viongozi wa CCM kwa kulitumia Jeshi la Polisi kuvuruga amani ya nchi, chama hicho kitakuwa cha mwisho kuelekea katika uvunjifu huo wa amani.
“Ndugu zangu Polisi watambue njia ya kuelekea amani ya kudumu ni kuheshimu demokrasia, wasitumie ofisi zao kunyanyasa, kuwatesa na kuwapiga wananchi, hali hii ikome kuanzia sasa,” alisema Mbowe.
Akitumia nukuu ya Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Mbowe alisema serikali yoyote inayotumia nguvu na majeshi kwa ajili ya kuulinda utawala wa kidhalimu, ndiyo inayowafundisha raia wa nchi hiyo kutumia nguvu kuwapinga.
Alisema harakati za mabadiliko yanayofanywa sasa na chama hicho kupitia kaulimbiu yao ya (M4C) ni maandalizi ya kushika dola mwaka 2015 na kuwataka wananchi kushiriki kwa kila namna katika harakati hizo.
Dk. Slaa atoa mikoba
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa alisema taifa lipo katika hali ngumu ikiwamo, mfumuko wa bei, unaosababisha kupanda kwa gharama za maisha kunakochangiwa na na matumizi mabaya ya serikali.
Alisema jambo jingine linalochangia hali ngumu ya maisha ni pamoja na rais kuwa na mamlaka makubwa ya uteuzi pasipo kushauriana na mtu, hali inayomfanya aonekane kama mungu mtu.
“Serikali ina matumizi makubwa kiasi cha kupelekea taifa katika umasikini na hakuna mwananchi wala wabunge kuhoji na akapatiwa jibu, kwani ukihoji unaambiwa mamlaka ya rais hayahojiwi, si wewe na mimi wala wabunge na mawaziri wake,” alisema Dk. Slaa.
Akielezea zaidi, Dk. Slaa alisema, rais amekuwa akigawa vyeo kwa kutumia mamlaka yake vibaya katika nafasi mbalimbali ikiwamo kwa waliompa hifadhi, marafiki, ndugu na wale waliomsaidia kuingia Ikulu huku akihoji ukubwa wa baraza la mawaziri.
Alitolea mfano Uingereza kuwa waziri mkuu, ana mamlaka ya kuchagua mawaziri 20 tu, na akizidisha zaidi ya hapo atalazimika kumlipa kwa hela yake ya mfukoni na si kodi za wananchi.
Aidha, aliwataka wabunge wa chama hicho kutetea masilahi ya wananchi watakapoingia katika Bunge la bajeti litakaloanza Juni 12 na kwamba kama watazomewa na watu wasitake wananchi watetewe, litakuwa ni jukumu la wananchi kuwazomea wakirudi katika majimbo yao.
Lissu
Ilipofika zamu ya Tundu Lissu kuzungumza, wananchi walimlazimisha avue kofia yake aina ya ‘Pama’ ili waweze kumuona na alipofanya hivyo wakalipuka kwa shangwe kwa kuimba ‘jembe, jembe, jembe’ hadi Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) aliposimama na kuwaomba watulie.
Akihutubia mkutano huo, Lissu alijikita katika suala zima la wananchi kufahamu umuhimu wa Katiba na kuweza kutoa maoni yatakayohitimisha utawala wa kichifu nchini.
Alisema licha ya suala hilo kupigiwa kelele na watu mbalimbali serikali ya CCM imekubali mchakato huo kwa hila huku ikitunga sheria hovyo ya kuupeleka bungeni, wakitumia wabunge waliopo kwa kuamini wapo wengi na hivyo watapitisha kwa masilahi yao na chama chao.
Aliongeza kuwa hata hatua ya kuzuia masuala ya muungano yasijadiliwe ni njia moja wapo ya matumizi mabaya ya madaraka, kwa kuwa suala hilo haliwezi kutenganishwa na Watanzania.
Aliwataka wananchi kuhakikisha tume ya maoni ya Katiba itakapowafikia wawe na ujasiri wa kuuliza nafasi ya Tanganyika katika Serikali ya Muungano kwa kile alichosema mpaka sasa baada ya Zanzibar kurekebisha katiba yao Tanzania haijulikani ina nchi ngapi, wakuu wa nchi wangapi na maamiri jeshi wangapi.
Alisisitiza Watanzania wasisite kutaka kuwepo kura ya maoni kuangalia kama yaliyofanyika Zanzibar ni sawa kwa ustawi mzima wa muungano.
Aidha, Lissu alisema kwa utaratibu wa sasa bunge litakapokaa kama bunge la katiba ni wazi CCM na washirika wake watakuwa zaidi ya 400 na kutaka suala hilo lihusishe watu wa kada mbali mbali pasipo kujali vyama vyao kwa ajili ya kupig kura hiyo katika bunge la katiba.
Akizungumzia mamlaka ya uteuzi, Lissu alisema yanatumika vibaya kwa kuwa katika Bunge tayari kuna theluthi moja ya wabunge ambao kazi yao ni kugonga meza kwa ajili ya kupongeza kila kitu kwa kuwa hawawajibiki kwa wanchi.
Lema
Aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini Godbles Lema, akizungumza katika mkutano huo alisema yupo kwenye ‘honeymoon’ na kwamba wakati wowote atarudi kazini kuwatumikia wananchi wa Arusha.
Alisema kwa hali ilivyo sasa siyo lazima kufika mwaka 2015 kama viongozi wa serikali wataendelea kufanya ubadhirifu unaosikika kila kunapokucha.
Alibainisha hali hiyo ya ubadhirifu ndiyo inayosababisha kuwepo na machangudoa, majambazi na hata omba omba licha ya kuwa ni nchi tajiri na inayoshika nafasi ya tatu kwa kuwa na almasi zilizo bora kidunia.
Naye Mbunge wa Ilemela, Ezekia Wenje, alisema nchi ya Tanzania ni kubwa kuliko Mtanzania yeyote aliyeko CHADEMA, CCM na hata vyama vingine na kwamba kila mmoja ana wajibu wa kutunza amani.
Kwa upande wake, Halima Mdee, alisema umati wa watu uliojitokeza katika mkutano huo unaashiria kuwa Dar es Salaam, hakukaliki kwa upande wa CCM, na kuondoa dhana waliyokuwa wakijivunia CCM kuwa Dar ni ngome yao.

CHANZO - Tanzania Daima
Kwa hisani ya chademablog.

Thursday, May 24, 2012

OFFICIAL: LLOYD NCHUNGA ABWAGA MANYANGA YANGA

LLOYD NCHUNGA BIHARAGU
C/O LLOYD ADVOCATES,
Morogoro/Bibi TIti  Mohamed Rd,7th Floor, J.K. Nyerere Pension towers
P.BOX 75111, Dar-Es- Salaam,Tanzania.


                                                                   

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUJIUZULU NAFASI YA UENYEKITI WA KLAB YA YANGA.
Ndugu wana Habari, najua kwamba taarifa hii itawafedhehesha wajumbe na wanayanga wanaotuunga mkono,hasa ukizingatia maamuzi ya pamoja ya vikao vyetu vya kamati ya utendaji vilivyopita kwamba hakuna wa kujiuzulu kati yetu mpaka tujue hatma ya mkutano mkuu ambao tulipanga ufanyike tarehe 15 Julai 2012, ukiachia mbali shinikizo la kujiuzulu linalotolewa na baadhi ya wazee na wanaojiita vijana wa klab, kwa wajumbe wa kamati ya utendaji, na hasa mimi kama mwenyekiti.
Nawashukuru wajumbe kwamba tulifanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mzuri, na hata pale tulipotofautiana tulifanya hivyo kwa hoja na kufikia maazimio ambayo wote tulikuwa tunawajibika nayo.
Tangu tumeingia madarakani tumeweza kushirikiana na kupata mataji matatu katika kipindi cha mwaka mmoja, yaani; Ngao ya Hisani 2010, Ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2010/2011, na Ubingwa wa  Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup), 2011. Zaidi ni kwamba tuliuwa uteja kwa watani wetu wa jadi kila tulipokutana katika ligi ukiachia mbali mechi ya tarehe 6 Mei 2012, ambayo tulifungwa goli 5 bila, na kuleta mtafaruku mkubwa katika klab yetu.
Hali kadhalika tumeshirikiana  mpaka tumeweza kuboresha mkataba kati yetu na TBL kupitia Kilimanjaro Premium Lager, tumeingia mkataba na  kampuni ya NEDCO  kuendeleza mali zetu katika mtaa wa mafia na uwanja wetu wa KAUNDA baada ya kufikia hatua nzuri katika kupata hati miliki za maeneo yote mawili. Nafahamu kwamba kampuni hiyo iko katika hatua za mwisho za kumalizia michoro.
Hali kadhalika tuliingia mkataba wa kuzalisha na kuuza bidhaa zenye nembo yetu na hasa baada ya kufanya marekebisho yatokanayo na matakwa ya sheria kule BRELA na pia mkataba na kampuni ya NEXUS LTD, ambayo itakuwa inatutafutia wadhamini wa nje na ndani, kufanya promosheni zetu na kampeni kwa njia ya electronic kupitia mitandao mbalimbali na kukusanya data za wanachama na kusajili  wapya tukiwa na malengo ya kukusanya shilingi 300,000,000/= hadi 800,000,000/= kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitatu. Haya yote tuliyafanya tukilenga kujitegemea kujazia mapengo yaliyokuwa yakitokana na kutegemea ufadhili wa mtu mmoja mmoja.
Kwa ridhaa yenu tumekua tukiendelea na mazungumzo na makampuni mbali mbali kwa ajili ya udhamini na kwa sababu maalum, nitazitaja katika hati ya makabidhiano kwa kiongozi ajaye.
Aidha, tumeshirikiana katika kufanya mambo mbali mbali ya kijamii, ikiwa ni pamoja na sikukuu ya kuadhimisha miaka 77 ya Yanga, sikukuu za pasaka, kuchangia jamii na waliokumbwa na maafa, na kongamano la vijana lililolenga kuwaamsha vijana kuitambua nafasi yao katika Yanga ikiwa ni pamoja na kupata azimio la kuanzisha SACCOSS ya Yanga, ambapo maombi yapo kwa msajili Manispaa ya Ilala.
Haya yote nayataja ikiwa ni kuwashukuru kwa ushirikiano na ikiwezekana muweze kuyakamilisha yaliyobaki ambayo mtaona yalikuwa mazuri.
Lakini pia tulipopata matatizo tulikuwa pamoja.  Nichelee kusema tu kwamba tulisimama pamoja baada ya kujiuzulu Makamu Mwenyekiti wetu Ndugu Davis Mosha na mjumbe wetu  ndugu Seif A. Seif, Ali Mayayi, na wengineo, kwani tulifungwa na katiba.Tulisimama pamoja pia katika suala la kujiuzulu ndugu Yusuf M. Manji, aliyekuwa mdhamini mteule na mfadhili mkuu ambaye sasa ameonyesha nia ya kurudi nanyi mkaridhia mkutane naye. Awali, tulitumia kila jitihada za kumrejesha lakini ikashindikana.
Hata hivyo doa limetupata baada ya kufungwa na watani wetu goli 5 bila, ambapo kuna wanachama wanaoelewa na wasioelewa kabisa.
Ninachokiona mimi ni usaliti wa hali ya juu uliombatana na matukio mbalimbali yaliyopita na yanayoendelea hadi kujaribu kupindua uongozi wa halali wa kidemokrasia. SIWATUHUMU WACHEZAJI MOJA KWA MOJA, isipokuwa  mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo ule na sasa, inaonyesha kwamba kulikuwa na usaliti mkubwa ambao sisi hatukuweza kuubaini mapema.
Sioni mantiki katika hoja kwamba wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho n.k.  Au ati mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo  tuvune bao 5!
Kwa wanaoijua Yanga, imewahi kuwa na madeni makubwa katika Hoteli mbali mbali, mawakala wa ndege n.k, na baadhi tumeyakuta na sisi tumekuja tukayalipa. Hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwepo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki, na bado wachezaji walicheza kwa morali.
Hata hivyo, utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatula kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuuondoa uongozi wa kidemokrasia.
Baada ya mapinduzi kushindikana na TFF kuonya kuhusu mapinduzi hayo, wazee kupitia msemaji wao , Mzee Akilimali wamesikika katika kipindi cha Michezo  cha Redio moja maarufu hapa nchini wakidai kwamba ni bora Yanga ishushwe daraja au kufungiwa kuliko mimi kuendelea kuongoza!
Hii imenikumbusha HEKMA ZA MFALME SELEMANI akiamulia ugomvi wa wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto naye akaamuru wamgawane nusu kwa nusu. Yule mwenye mtoto kweli alimuomba Mfalme amuachie mwenzie kuliko kumkata nusu.
Kwa hekma hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika Uenyekiti  wa Yanga kwani ni klab ninayoipenda hata kama sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.
Vile vile siko tayari kuona klab yangu ikisalitiwa au kuhujumiwa eti kwa sababu tu mimi ni kiongozi.
Natumaini kamati ya utendaji kwa pamoja na wale tuliowateua chini ya ibara ya 29(3) ya katiba ya Yanga pamoja na bodi ya wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka kufikia mkutano mkuu kwa  mafanikio zaidi.
 Nitaendelea kuwa mwanachama mwadilifu na nitatoa mchango wangu wa hali na mali pale nitakapo hitajika na nikiwa  na uwezo wa kufanya hivyo.
YANGA DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.
Wasalaam,


LLOYD NCHUNGA BIHARAGU.

Nakala kwa:-
Mama Fatma Karume,Mdhamini
Francis Kifukwe, Mdhamini
Bwana Yusuf Manji – Kwa taarifa 
Kwa hisani ya Shaffih Dauda
 MH.MNYIKA ASHINDA KESI.
Mh. Mnyika ashinda kesi baada ya Jaji kuzitupili mbali hoja zote tano.



HOJA zenyewe ni hizi:
1)Kwamba Mnyika alimtuhumu kuuza nyumba za UWT
2)Kutumia Laptop za Mnyika Kuhesabu kura
3)Kuingia watu wengi wa CHADEMA ktk chumba cha kuhesabia kura
4)Kuzidi kwa kura hewa 16,000
5)Kukosewa kwa karatasi za kujumulisha kura (form)
HONGERA MH.MNYIKA, HONGERENI CHADEMA TURUDI TUTEKELEZE AHADI ZETU.

Monday, May 21, 2012

SIMBA YAMUONGEZEA MKATABA PROF; CIRCOVIC

Kufuatia mafanikio mazuri aliyoyapata kocha mkuu wa wekundu wa msimbazi Prof. Milovan Circovic Club ya soka ya simba imemuongezea mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi hicho kuanzia sasa. Uongozi wa Simba umesema kipimo kikubwa cha kocha ni vikombe na kandanda safi ki2 ambacho wanaridhishwa na mwenendo wa timu chini ya Milovan huku akifanikiwa kumfunga mtani wa jaji mabao 5-0.

Wednesday, May 16, 2012

PATRIC MUTESA MAFISANGO IS NO MORE;










 
 
 
 
Jembe amefariki dunia maeneo ya Tazara akiwa na familia yake walikuwa wanatokea maisha club, na alipofika Tazara bodaboda mmoja akatokea ghafla na alipojaribu kumkwepa ndipo ajali ikamkuta na kusababisha kifo chake, R.I.P Patrick Mutesa Mafisango tutakukumbuka daima.
POLENI WANA SIMBA WENZANGU NA WAPENDA SOKA WOTE KWA UJUMLA, MUNGU AMUWEKE MAHALI PANAPOMSTAHILI. 
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



PATRICK Mutesa Mafisango (32), mchezaji tegemeo wa Simba SC amefariki dunia jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo katika eneo la Keko jirani na Chuo cha VETA jijini Dar es Salaam.
Mafisango alikufa kutokana na ajali iliyotokea wakati gari alilokuwa akiendesha lilipogonga mti ulio pembezoni mwa barabara ya Chang’ombe majira ya saa kumi kasorobo alfajiri. Marehemu alifariki papo hapo.
Kwenye gari aliyokuwamo Mafisango, kulikuwapo na abiria wengine wanne lakini ni Mafisango pekee ndiye aliyefariki dunia.
Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tayari kwa kusafirishwa kwenda kwao Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambako atazikwa.
Ingawa alikuwa na uraia wa Rwanda na akiichezea timu ya taifa ya nchi hiyo (Amavubi), Mafisango alikuwa ni mzaliwa na raia wa DRC na uamuzi wa kuzikiwa huko ni wa familia yake.
Msiba wa Mafisango uko katika eneo la Keko Toroli jirani na kituo cha Chang’ombe Maduka Mawili (Njia Panda Sigara).
Mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa kesho Ijumaa saa nne asubuhi katika viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda Kinshasa majira ya saa kumi jioni.
Mafisango alizaliwa Machi 30, 1980 huko Kinshasa Zaire wakati huo na ameacha mke na mtoto mmoja wa kiume, Chris Paul, mwenye umri wa miaka mitano.
Mafisango ameichezea Simba kwa msimu mmoja tu akitokea Azam ya Dar es Salaam lakini kabla ya hapo alichezea pia TP Mazembe ya DRC, APR ya Rwanda na pia aliwahi kuwa nahodha wa Amavubi kwa takribani miaka mitano.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, Makamu wake, Geofrey Nyange Kaburu na wajumbe wa kamati ya watendaji wameeleza kusikitishwa kwao na msiba huu mkubwa kwa klabu na wamewataka wana Simba wote kuwa watulivu na kumwombea marehemu Mungu amlaze mahali pema peponi.
Uongozi wa Simba unaahidi kuwa utatoa taarifa nyingine zozote muhimu kwa wananchi ili wafahamu kuhusu msiba huu pale itakapotokea.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC
17/5/2012

Monday, May 14, 2012

Kim amuita Boban, Bocco, Sama goal Stars

KOCHA Mkuu wa ya soka ya taifa ya Tanzania, Taita Stars, Kim Poulsen leo (Mei 14 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast.

Akitangaza kikosi hicho ambacho kitaingia kambini kesho kutwa (Mei 16 mwaka huu, Kim amesema uteuzi wake umezingatia uwezo wa mchezaji uwanjani, nafasi anayocheza na ubora wake.

Wachezaji walioitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar).

Mabeki ni Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).

Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).

Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United-U20), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam).

Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi kabla kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.

Friday, May 11, 2012

 TFF YAMTANGAZA KIM POULSEN KUWA KOCHA MPYA STARS










Release No. 072
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 11, 2012
KIM KOCHA MPYA TAIFA STARS
Kim Poulsen ameteuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania (Taifa Stars) kuanzia Mei 11 mwaka huu kuziba nafasi ya Jan Poulsen.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema Kim amepewa mkataba wa mwaka mmoja baada ya Shirikisho kuamua kutomuongezea mkataba Jan. Mkataba wa Jan uliokuwa wa miaka miwili unamalizika Julai 30 mwaka huu.
Amesema kwa vile Taifa Stars inakabiliwa na mechi za mchujo za Kombe la Dunia raundi ya pili Kanda ya Afrika na mechi za mchujo za Kombe la Mataifa ya Afrika (CAN), TFF imeona ni lazima iwe na kocha mpya mapema kabla ya mkataba wa Jan kumalizika.
Kim ambaye ni raia wa Denmark amekuwa nchini kwa mwaka mmoja sasa akifundisha timu za Taifa za vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) na miaka 20 (Ngorongoro Heroes), hivyo anawafahamu vizuri wa wachezaji wa Tanzania.
TFF imeanza mchakato wa kutafuta kocha mwingine wa timu za vijana atakayeziba nafasi ya Kim. Ili kuwa na makocha wenye falsafa moja, kocha huyo anatafutwa kutoka Denmark.
Naye Kim ambaye Jumatatu (Mei 14 mwaka huu) atatangaza kikosi cha Taifa Stars ambacho Juni 2 mwaka huu kuivaa Ivory Coast katika mechi ya mashindano amesema yuko tayari kwa kazi hiyo na kusisitiza kuwepo ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali ili timu hiyo iweze kufanya vizuri.
RAMBIRAMBI MSIBA WA MWANDISHI RACHEL MWILIGWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu) katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa miguu kwani Rachel kwa kipindi chote akiwa mwandishi na baadaye Mhariri alikuwa akifanya kazi nasi, hivyo mchango wake katika mpira wa miguu tutaukumbuka daima.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Rachel, kampuni ya New Habari ambayo ndiyo inayomiliki gazeti za Mtanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Mungu aiweke roho ya marehemu Rachel mahali pema peponi. Amina
TWIGA STARS, ZIMBABWE KUUMANA LEO
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake ya Tanzania (Twiga Stars) na Zimbabwe zinapambana kesho (Mei 12 mwaka huu) katika mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Twiga Stars ambayo ilikuwa katika ziara ya mechi za kirafiki katika mikoa ya Dodoma na Mwanza imerejea leo (Mei 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam tayari kuikabili Zimbabwe. Ikiwa Mwanza jana ilicheza mechi ya kirafiki dhidi Rock City Queens, lakini mechi hiyo ilivunjika dakika ya 58 kutokana na mvua kubwa. Hadi mechi inavunjika, Twiga Stars ilikuwa ikiongoza kwa mabao 5-0.
Kwa mujibu wa kocha wa Twiga Stars, Charles Boniface Mkwasa, mechi hiyo itakuwa kipimo kizuri kwao kabla ya kucheza mechi ya mashindano ya Afrika (AWC) dhidi ya Ethiopia. Mechi hiyo itachezwa Mei 26 mwaka huu jijini Addis Ababa kabla ya kurudiana Dar es Salaam wiki mbili baadaye.
Naye Kocha wa Zimbabwe, Rosemary Mugadza amesema amefurahi kupata mechi hiyo kwa vile anaamini Twiga Stars ni kipimo kizuri kwao kabla ya kucheza mechi yao ya AWC dhidi ya Nigeria.
Twiga Stars na Zimbabwe zilishakutana mara mbili mwaka jana. Mara ya kwanza ilikuwa nusu fainali ya Kombe la COSAFA ambapo katika mechi hiyo iliyochezwa Julai 5 jijini Harare, Zimbabwe ilishinda kwa penalti 4-2.
Mechi ya pili ilikuwa michezo ya All Africa Games (AAG) iliyofanyika Maputo, Msumbiji ambapo timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
Viingilio katika mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi wa kimataifa Judith Gamba kuanzia saa 10.30 jioni ni sh. 1,000 tu kwa sehemu zote isipokuwa VIP A ambayo ni sh. 10,000 na VIP B ambayo kiingilio chake ni sh. 5,000.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Wednesday, May 9, 2012

UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA WAPYA WAKAMILIKA



Waziri Mkuu Mheshimiwa MIZENGO PINDA ametangaza Wakuu wapya wa Wilaya huku Wakuu wa Wilaya 51wa zamani akiwaacha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya kustaafu kazi.
Akitangaza Wakuu hao wapya wa Wilaya mbele ya Wahariri wa vyombo vya habari nchini, Waziri Mkuu amesema kati ya Wakuu hao wa Wilaya 133 walioteuliwa wapya ni Sabini wakiwemo Waandishi wa habari Sita.

Kulingana na Waziri Mkuu kabla ya kutangazwa kwa Wilaya mpya kulikuwa na Wakuu wa Wilaya 114 ambapo kati ya Wakuu hao wa Wilaya wa Zamani 63 wamebaki katika uteuzi wa leo na 51 wameachishwa kazi.

mkuu wa wilaya mkoa wa Mbeya aliyetangaza kujiuzulu atemwa rasmi





MAJINA YA WAKUU WA WILAYA WAPYA 70 NA VITUO VYAO VYA KAZI
-
  
NA.
KITUO CHA KAZI
1.Novatus MakungaHai
2.Mboni M. MgazaMkinga
3.Hanifa M. SelunguSikonge
4.Christine S. MndemeHanang
5.Shaibu I. NdemangaMwanga
6.Chrispin T. MeelaRungwe
7.Dr. Nasoro Ali HamidiLindi
8.Farida S. MgomiMasasi
9.Jeremba D. MunasaArumeru
10.Majid Hemed MwangaLushoto
11Mrisho GamboKorogwe
12.Elias C. J. TarimoKilosa
13.Alfred E. MsovellaKiteto
14.Dkt. Leticia M. WariobaIringa
15.Dkt. Michael Yunia KadegheMbozi
16.Mrs. Karen YunusSengerema
17.Hassan E. MasalaKilombero
18.Bituni A. MsangiNzega
19.Ephraem Mfingi MmbagaLiwale
20.Antony J. MtakaMvomero
21.Herman Clement KapufiSame
22.Magareth Esther MalengaKyela
23.Chande Bakari NalichoTunduru
24.Fatuma H. ToufiqManyoni
25.Seleman LiwowaKilindi
26.Josephine R. MatiroMakete
27.Gerald J. GuninitaKilolo
28.Senyi S. NgagaMbinga
29.Mary TeshaUkerewe
30.Rodrick MpogoloChato
31.Christopher MagalaNewala
32.Paza T. MwamlimaMpanda
33.Richard MbehoBiharamulo
34.Jacqueline LianaMagu
35.Joshua MirumbeBunda
36.Constantine J. KanyasuNgara
37.Yahya E. NawandaIramba
38.Ulega H. AbadallahKilwa
39.Paul MzindakayaBusega (mpya)
40.Festo KiswagaNanyumbu
41.Wilman Kapenjama NdileMtwara
42.Joseph Joseph MkirikitiSongea
43.Ponsiano NyamiTandahimba
44.Elibariki Immanuel KinguKisarawe
45.Suleiman O. KumchayaTabora
46.Dkt. Charles O. F. MlingwaSiha
47.Manju MsambyaIkungi (mpya)
48.Omar S. Kwaangw’Kondoa
49.Venance M. MwamotoKibondo
50.Benson MpesyaKahama
51.Daudi Felix NtibendaKaratu
52.Ramadhani A. ManenoKigoma
53.Sauda S. MtondooRufiji
54.Gulamhusein KifuMbarali
55.Esterina KilasiWanging’ombe (mpya)
56.Subira MgaluMuheza
57.Martha UmbulaKongwa
58.Rosemary KiriginiMeatu
59.Agness HokororoRuangwa
60.Regina ChonjoNachingwea
61.Ahmed R. KipoziBagamoyo
62.Wilson Elisha NkhambakuKishapu
63.Amani K. MwenegohaBukombe
64.Hafsa M. MtasiwaPangani
65.Rosemary Staki SenyamuleIleje
66.Selemani Mzee SelemaniKwimba
67.Lt. Col. Ngemela E. LubingaMlele (mpya)
68.Iddi KimantaNkasi
69.Muhingo RweyemamuHandeni
70.Lucy MayengaUyui

MAJINA 63 WAKUU WA WILAYA WA ZAMANI NA VITUO VYAO VYA KAZI

NA.JINAKITUO CHA KAZI
1.James K. O. MillyaLongido
2.Mathew S. SedoyekaSumbawanga
3.Fatuma L. KimarioIgunga
4.Capt. (Mst.) James C. YamunguSerengeti
5.Lt. (Mst.) Abdallah A. KihatoMaswa
6.Sarah DumbaNjombe
7.Jowika W. KasungaMonduli
8.Elizabeth C. MkwasaBahi
9.Col. Issa E. NjikuMisenyi
10.John B. HenjeweleTarime
11.Elias W. LaliNgorongoro
12.Raymond H. MushiIlala
13.Francis MitiUlanga
14.Evarista N. KalaluMufindi
15.Mariam S. LugailaMisungwi
16.Anna J. MagowaUrambo
17.Anatory K. ChoyaMbulu
18.Fatma Salum AllyChamwino
19.Deodatus L. KinawiroChunya
20.Ibrahim W. MarwaNyang’hwale (mpya)
21.Dkt. Norman A. SigallaMbeya
22.Moshi M. Chang’aMkalama (mpya)
23.Jordan M. RugimbanaKinondoni
24.Georgina E. BundalaItilima (mpya)
25.Halima M. KihembaKibaha
26.Manzie O. MangochieGeita
27.Abdula S. LutaviNamtumbo
28.Zipporah L. PanganiBukoba
29.Dkt. Ibrahim H. MsengiMoshi
30.Col. Cosmas KayomboKakonko (mpya)
31.Lembris M. KipuyoMuleba
32.Elinasi A. PallangyoRombo
33.Queen M. MloziSingida
34.Juma S. MadahaLudewa
35.Angelina MabulaButiama (mpya)
36.Hadija H. NyemboUvinza (mpya)
37.Ernest N. KahindiNyasa (mpya)
38.Peter T. KiroyaSimanjiro
39.John V. K. MongellaArusha
40.Baraka M. KonisagaNyamagana
41.Husna MwilimaMbogwe (mpya)
42.Sophia E. MjemaTemeke
43.Francis IsaacChemba (mpya)
44.Abihudi M. SaideyaMomba (mpya)
45.Khalid J. MandiaBabati
46.Anna Rose NyamubiShinyanga
47.Dani B. MakangaKasulu
48.Amina J. MasenzaIlemela
49.Mercy E. SillaMkuranga
50.Christopher R. KangoyeMpwapwa
51.Lt. Edward O. LengaKalambo (mpya)
52.Halima O. DendegoTanga
53.Lephy B. GembeDodoma
54.Saidi A. AmanziMorogoro
55.Jackson W. MsomeMusoma
56.Elias C. B. GoroiRorya
57.Lt. Col. Benedict KitengaKyerwa (mpya)
58.Erasto SimaBariadi
59.Nurdin H. BabuMafia
60.Khanifa M. KaramagiGairo (mpya)
61.Gishuli M. CharlesBuhigwe (mpya)
62.Saveli M. MakettaKaliua (mpya)
63.Darry RwegasiraKaragwe

 
NA
OFISI YA WAZIRI MKUU,
DAR ES SALAAM.
9 MEI 2012