Simba tunu ya Afrika Mashariki
Kwa mujibu wa tovuti ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Simba ndiyo timu pekee ya Afrika Mashariki ambayo imebaki katika michuano ya makombe yanayosimamiwa na Shirikisho hilo.
Kwa mujibu wa tovuti hiyo, hakuna timu kutoka katika jumuiya hiyo ambayo bado ipo katika michuano hiyo ukiondoa Simba SC. Nchi tano zinaunda Jumuiya hiyo ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Orodha hiyo inaonyesha kwamba nchi ya Sudan ndiyo kinara kwa ngazi ya vilabu barani Afrika kufikia sasa baada ya kuingiza timu nne katika michuano ya Ligi ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la CAF.
Timu ambazo Sudan imeingiza katika michuano hiyo ni El Merreikh na Al Hilal ambazo zimesonga mbele katika Ligi ya Mabingwa na Al Ahly Shandy na El Amal ambazo zimesonga mbele katika Kombe la Shirikisho (CAF).
Shandy ndiyo timu ambayo itacheza na Simba katika hatua ya 16 bora baadaye mwezi huu.
Casinos In Dubai - Airport Review & Hotels - Air
ReplyDeleteBook where can you buy air jordan 18 retro red suede a Flight or authentic air jordan 18 retro yellow suede Flight On Airfare & Book Direct In Dubai (Tif) with Airjet air jordan 18 retro red to good site Radar, Free Shipping or Book Direct Direct On Airfare air jordan 18 retro men blue online shop and Book Direct air jordan 18 retro yellow suede super site In Dubai.